• MUHIMU

    NDUGU MSOMAJI WETU ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU SASA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO/MUZIKI WAKO NASI KWA BEI NAFUU SANA AMBAYO ITAKUFANYA UWIFIKIWE NA WATEJA WENGI NCHINI.PIA TUNATOA HUDUMA ZA BLOG DESIGN NA ANDROID APLLICATION TUPIGIE 0655569428 AU FOLLOW INSTAGRAM @star255com FACEBOOK:sta255 TWITTER: star255_ KARIBUNI SANA.>>

    TID KUACHIA ‘MAISHA YA JELA’ FT FID Q



    Wimbo huo ulirekodiwa mwaka 2007, siku tatu tu baada ya muimbaji huyo kutoka jela. Kutoka jela kwa muimbaji huyo kulitokana msamaha wa Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete siku ya Uhuru.
    Maisha ya Jela unazungumzia msoto ambao muimbaji huyo aliupata baada ya kufungwa jela. “TID ameelezea maumivu, maumivu ya moyo, kuchanganyikiwa, na bila kusahau mateso ya kiakili aliyoyapata akiwa jela kutokana na adhabu kali alizozipata baada ya hukumu hiyo,” yanasema maelezo.
    Fid Q alikuwa mtu wa karibu na TID wakati wa kifungo na baada ya kutoka na alimwelezea namna wananchi walivyochukulia kufungwa kwake hivyo alikuwa mtu sahihi kushirikishwa kwenye wimbo huo ambao ulikuwa wazo na CEO wa Tongwe Records, J-Murder.
    Hata hivyo licha ya wimbo huo kumalizika, haukuweza kutoka kipindi hicho kwasababu walitaka kwanza TID awe kwenye hali ya kawaida baada ya kutoka kifungoni.
    Bado haijatajwa tarehe rasmi ya kutoka kwa wimbo huo. Hivi karibuni TID alikiri kuwa mmoja wa waathiriwa wa matumizi ya dawa za kulevya.

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad