• MUHIMU

    NDUGU MSOMAJI WETU ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU SASA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO/MUZIKI WAKO NASI KWA BEI NAFUU SANA AMBAYO ITAKUFANYA UWIFIKIWE NA WATEJA WENGI NCHINI.PIA TUNATOA HUDUMA ZA BLOG DESIGN NA ANDROID APLLICATION TUPIGIE 0655569428 AU FOLLOW INSTAGRAM @star255com FACEBOOK:sta255 TWITTER: star255_ KARIBUNI SANA.>>

    KOTEI: MSUVA NI NOMA SANA


    Kiungo wa Simba, Mghana, James Kotei, amechungulia katika kikosi cha Yanga na kusema: “Simon Msuva ndiye mchezaji bora kwa upande wa Yanga.”  
    Kotei ameyasema hayo baada ya kuisaidia timu yake ya Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
    Kotei amesema ushindi walioupata dhidi ya Yanga haumaanishi kwamba wapinzani wao hawakuwa vizuri, bali waliwazidi kidogo na kutumia udhaifu wao.
    “Yanga walikuwa wazuri na ndiyo maana waliweza kutufunga kabla ya sisi kusawazisha na kuwaongeza, kikubwa pointi tatu tulizozipata ni juhudi zetu binafsi hasa ukizingatia tulikuwa pungufu.
    “Katika mchezo wetu huu, Yanga nimeona ilikuwa na mchezaji mmoja tu mzuri, yule aliyevaa jezi namba 27 (Msuva) kwani alikuwa akitusumbua sana kuliko wachezaji wengine wote wa Yanga,” alisema Kotei. 

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad