• MUHIMU

    NDUGU MSOMAJI WETU ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU SASA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO/MUZIKI WAKO NASI KWA BEI NAFUU SANA AMBAYO ITAKUFANYA UWIFIKIWE NA WATEJA WENGI NCHINI.PIA TUNATOA HUDUMA ZA BLOG DESIGN NA ANDROID APLLICATION TUPIGIE 0655569428 AU FOLLOW INSTAGRAM @star255com FACEBOOK:sta255 TWITTER: star255_ KARIBUNI SANA.>>

    WANAFUNZI 8000 HATARINI KUFUTIWA VYUO VIKUU



    Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema zaidi ya wanafunzi 8,000 wa vyuo vikuu 52 nchini wapo njia panda ya kuendelea na masomo baada ya uhakiki kukamilika.

    TCU ilitoa taarifa yake Jumatano hii kwa vyombo vya habari, kuwa imewabaini wanafunzi ambao wamedahiliwa katika programu ambazo hawana sifa. Orodha ya wanafunzi hao tayari imewasilishwa kwenye vyuo vikuu vya Dar es Salaam (UDSM), Dodoma (UDOM), Mtakatifu Augustine (SAUTI) na Tumaini.
    Aidha taarifa hiyo imebainisha kuwa orodha ya wanafunzi wasio na sifa imeshawasilishwa kwenye vyuo husika.”Hivyo wanafunzi wote wanaoendelea na masomo kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini wanaweza kutazama matokeo ya uhakiki wao kupitia tovuti ya tume,” ilisema taarifa hiyo kupitia tovuti ya tume hiyo.
    Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alilotoa mwaka jana, mwezi Agosti baada ya kutangaza kuwapo kwa wanafunzi ‘hewa’ ambao wanapatiwa mikopo na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad