LINAH AJUTIA UJAUZITO WAKE
Msanii wa bongo Fleva Linah Sanga huenda hajapenda mabadiliko ya mwili wake baada ya kupata ujauzito kwani mwili wake kwa sasa shepu yote imetoweka kiasi kwamba anakumbuka kama sio ku’miss umbo lake la zamani.
Linah kupitia ukurasa wake wa Instagram ameposti picha ya zamani akionesha umbo lake lilivyokua zuri enzi hizo na kuandika “Siku za nyuma, dah! Sijui mwili wangu utarudi hivyo“
Ingawaje hata hivyo mashabiki wake wengi wameonekana kuguswa na kilio chake na kumpa ushauri kuwa ajitahidi mazoezi pindi atakapojifungua na kula mboga za majani.

No comments