UZINDUZI WA ALBUM YA WOMAN YA LADY JAYDEE KUFANYIKA IJUMAA
Mwanamuziki na mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva Judith Wambura Mbibo a.k.a Lady JayDee yuko mbioni kufanya uzinduzi wa album yake ya 7 siku ya tarehe 31 ya mwezi huu inayokwenda kwa jina WOMAN.
Akizungumza na Global Publisher Lady Jaydee amesema kuwa kufika sasa hana msanii yoyete atakayemsindikiza katika show yake hiyo ya uzinduzi ambapo mbali na uzinduzi huo ataambatanisha na kurudi kwa urushaji wa kipindi chake cha Tv cha Diary ya Lady JayDee.
“namkaribisha mtu yeyote, msanii yeyote ambaye ataguswa na kuona kuwa anataka kuwa sehemu ya onyesho hili lakini mpaka sasa siwezi kusema kuwa kuna msanii yeyote ambaye atanisindikiza kwenye show yangu”Alisema Lady JayDee.
Hata hivyo Lady JayDee amesema msanii yeyote imwenye uwezo wa kufanya kazi ya sanaa ameruhusiwa kujumuika naye katika kuhakikisha mafanikio ya uzinduzi hiyo utakaofanyika katika ukumbi wa Lugalo Golf Club.

No comments