DIAMOND NA AY WAFANYA KUFURU YA PESA
Ukizungumzia watu maarufu kuongeza vitu vya ziada na mbwenbwe kwenye magari yao wanayotumia alimaarufu kama Car Pimping ni jambo linalozidi kushika kasi kiasi kwamba hata watu wasio maarufu wanashiwishika kufanya hivyo na Dicksound mmoja kati ya mhusika wa mambo hayo bila kuficha awataja mastaa wa bongo walioweka kiasi kikubwa cha pesa kwenye kuongeza vitu vya ziada kwenye magari wanayotumia.
Dicksound amewataja Diamond na Ambwene Yessaya ‘AY’ kuwa ni watu maarufu waliolipia kiasi kikubwa cha pesa ili magari yao yaongezwa vitu vya ziada.
“aliyewahi kuweka pesa ndefu alikuwa diamond ambaye nilimfungia kwenye Harrier ambayo muziki ulikuwa mkubwa sana baadae kwa msanii wa kiume aliyeweka mpunga mkubwa kwenye gari yake na kuipimp vizuri ni AY kwasasa hivi kwasababu mi ndo ambaye magari yao wote nayafanyia kazi”Alisema Dicksound alipokuwa akizungumza na Sam Misago Tv.
Hata hivyo akizungumzia upande wa mastaa wa kike kufanya car pimping amesema kuwa mara nyingi hawahitaji vitu vikubwa bali wao umependa mapambo enye rangi pendwa za kike hasa hasa ndani ya magari.

No comments