• MUHIMU

    NDUGU MSOMAJI WETU ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU SASA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO/MUZIKI WAKO NASI KWA BEI NAFUU SANA AMBAYO ITAKUFANYA UWIFIKIWE NA WATEJA WENGI NCHINI.PIA TUNATOA HUDUMA ZA BLOG DESIGN NA ANDROID APLLICATION TUPIGIE 0655569428 AU FOLLOW INSTAGRAM @star255com FACEBOOK:sta255 TWITTER: star255_ KARIBUNI SANA.>>

    HAMORAPA ANUSURIKA KUPIGWA CHUPA

    Usiku wa Jumamosi hii Harmorapa amenusurika kujeruhiwa vibaya na chupa wakati alipokuwa akitumbuiza katika ukumbi wa Maisha Basement uliopo Kijitonyama katika usiku wa Komela.


    Akiongea na kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio leo, meneja wa rapper huyo Irene Sabuka amesema, Harmorapa alirushiwa chupa lakini kwa bahati nzuri alikwepa la sivyo yangekuwa yanazungumzwa mengine.
    “Kiukweli hili jambo la kusikitisha sana, Harmorapa alikuwa stejini ana perfom ila kabla ya kumaliza show alitokea mtu mmoja akarusha chupa stejini bahati nzuri Harmorapa alikwepa ile chupa. Laiti asingekwepa au ingemkuta kwa bahati mbaya sasa hivi tungekuwa tunazungumza mengine,” amesema meneja huyo.
    “Mimi naona kile kitendo ni wivu tu sababu watu hawajui maisha kila mtu ana namna yake anayotokea. Harmorapa ametokea mtaani anatafuta maisha yake leo anaibuka mtu anamrushia chupa na kutaka kumjeruhi, anaibuka mtu mwingine anasema kuwa anataka kumuonesha na kukomesha,” ameongeza.

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad