• MUHIMU

    NDUGU MSOMAJI WETU ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU SASA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO/MUZIKI WAKO NASI KWA BEI NAFUU SANA AMBAYO ITAKUFANYA UWIFIKIWE NA WATEJA WENGI NCHINI.PIA TUNATOA HUDUMA ZA BLOG DESIGN NA ANDROID APLLICATION TUPIGIE 0655569428 AU FOLLOW INSTAGRAM @star255com FACEBOOK:sta255 TWITTER: star255_ KARIBUNI SANA.>>

    WAFUKUZWA KAZI KWA MAGUNIA 10 YA BANGI KILIMANJARO




    Baada ya Mahakama ya Kijeshi kuwatia hatiani polisi wanane mkoani Kilimanjaro kwa kukamata magunia 10 ya bangi na kuyaachia, wamefukuzwa kazi.
    Tukio hilo la polisi kukamata bangi hiyo, lilitokea Oktoba mwaka jana likihusisha askari wa Kituo cha Polisi Sanyajuu wilayani Siha.
    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kuchukua hatua hizo baada ya kuridhika na tuhuma dhidi yao.
    “Ni kweli kama ulivyopata hizo taarifa. Nimechukua uamuzi huo baada ya kuthibitishwa walikamata magunia 10 ya bangi na kuyaachia. Yule mkaguzi suala lake tumelipeleka juu,” amesema.
    Polisi waliofukuzwa kazi kwa fedheha ni:-

    1.Sajenti Sadick D.6004, 
    2.Koplo Innocent (D.9830), 
    3.Koplo Deusdedit (E.1703), 
    4.Koplo Semu (E.7525), 
    5.Koplo Salum (E.8907), 
    6.PC Kiroga (F.8983), 
    7.PC Filbert (F.8385) na 
    8.PC Ramadhan (G.3222).

    SOURCE: THOBIASOMEGA.COM

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad