HARMONIZE NA WOLPER WAMWAGA MAPENZI YAO HADHARANI
Msanii wa Bongo Fleva Rajab Abdul a.k.a Harmonize aliyechini ya usimamizi wa lebo ya WCB ameliweka wazi suala la watu kudhani kuwa anaishi na Jackline Wolpere kama mke na mme.
Akizungumza kupitia XXL ya Cloud Fm alizikubali tetesi za wawili hao kutokuwa sawa hapa katikati kimapenzi kuwa ni kweli kuna mambo ya kibinadamu yalitokea na kwasasa kila mmoja ametambua udhaifu wa mwenzake lakini mambo yanaenda sawa. kwasasa
Hata hivyo Harmonize amabainisha kutoishi pamoja na Wolper na kusema kuwa Jackline anaishi kwake na Harmonize anaishi kwake na mama yake na kila mtu anapomhitaji mwenzake wanawasiliana kuona uwezekano wa wao kuonana/kukutana.

No comments