HII NDIYO SABABU YA MR. NICE KUHAMIA KENYA
Huwezi kuwataja wakongwe waliofanya poa kipindi cha nyuma kwenye muziki wa Bongo FLeva ukaacha kumtaja Mr Nice.
Kwasababu ni mmoja kati ya wakongwe ambao walifanikiwa kuwa na fanbase kubwa sana kipindi cha nyuma, ila ukweli usiofichika ni kwamba mkali huyo kwasasa hana tena nguvu kama aliyokuwa nayo zamani kwa hapa nchini.
Star255 imeona sio kesi kama ikimtafuta Mr Nice na kupiga naye story kuhusu muziki wake na mambo mengine kibao. Na tumefanikiwa kuzungumza mambo mengi sana na mkali huyo ikiwa ni pamoja na maisha yake, muziki wake na vitu kama hivyo.
Mr Nice ameiambia star255 kwamba kwasasa ameamua kuhamishia makazi yake nchini Kenya, kwasababu ndio sehemu ambayo anaona anapata heshima kama msanii tofauti na Tanzania.
Pia Mr Nice amefunguka kuwa nchini Kenya ndio sehemu ambayo ana mashabiki wengi na muziki wake anaufanya poa kabisa na hata akiwa na show anapiga nyomi

No comments